Dar es Salaam. Shirika la Kimataifa la utafiti wa tiba na afya barani Afrika (Amref) limesema litaendelea kutoa hamasa na kuhakikisha kina mama wanapata huduma bora za afya wakati wa ujauzito hadi kujifungua.
Juzi shirika hilo kwa kushirikiana na Benki ya Azania (ABL), Kupitia kampeni yake ya ‘Stand up for African Mothers’ (SU4AM) jana lilifanya matembezi ya hisani yaliyohusisha viongozi wa Serikali na wananchi ili kukusanya Sh1 bilioni zitakazosaidia upatikanaji wa wakunga katika vituo vya afya nchini.
Akizungumza katika viwanja vya Green Grounds, Oysterbay jijini hapa mara baada ya matembezi Mkurugenzi mkazi wa Amref Dk Florence Temu alisema uwepo wa wakunga wenye utaalamu katika vituo vya afya utapunguza au kuepusha vifo vinavyotokea wakati wa kujifungua.
“Wakunga ni kiungo muhimu katika kutoa huduma stahiki za afya hasa ya uzazi wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua. Tunaomba na kuwasihi wananchi wote, mashirika, kampuni binafsi na washirika wa maendeleo, kuendelee kuchangia ili kufanikisha hili la kuokoa maisha ya mama na mtoto katika maeneo yenye uhitaji,” alisema.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa ABL, Charles Itembe , alisema benki hiyo kusaidia sekta ya afya, hasa katika afya ya uzazi ni moja ya nguzo za msingi za sera ya uwajibikaji wa kijamii.
“Wanawake ni nguzo ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi, bila ya huduma bora za afya na za msingi, wanawake katika nchi zinazoendelea kama Tanzania wataendelea kupotea maisha kwa vifo vya uzazi hali itakayosababisha kuzorota kwa maendeleo,” alisema Itembe.
Article first published on https://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Amref-yasisitiza-uwepo-wa-wakunga-kila-kituo-cha-afya/1597296-5177268-hu4agz/index.html
When Frederik Lokeun looks across the grounds of St. Matthews Nadome Primary School near Kakuma…
The influx of people, equipment and supplies needed to respond to the Ebola virus outbreak…
The current Ebola outbreak in East Africa is a stark reminder of how far the…
We have seen this happen way too many times in health systems; national policies are…
Kenya has made tremendous strides in reaching zero-dose children through a system-wide shift driven by…
Sometimes the biggest breakthroughs in health programmes do not come from new technologies or larger…