Categories: News

Mkakati mpya kumaliza Ukimwi 2030

Uzinduzi wa mradi huo ujulikanao Afya kamilifu ulifanyika  Maruhubi Mjini Zanzibar na kuzinduliwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Zanzibar, Asha Abdallah Ali.

Akizungumza baada ya kuzindua mradi huo, alisema Serikali itaendelea kuunga mkono jitihada za shirika hilo lenye lengo la kupambana na Ukimwi Zanzibar.

Aliliomba shirika hilo kuongeza nguvu zaidi katika makundi maalum kwa kuwa bado maambukizi ni makubwa kulinganisha na watu wa kawasaidia.

Aliyataja makundi hayo ni watumiaji wa dawa za kulevya wanaojidunga sindano, wanawake wanaofanya biashara ya ngono na wanaume wanaofanya mapenzi ya jinsia moja.

Aidha, alisema Zanzibar ina asilimia moja ya kiwango cha maambukizi na hiyo inatokana na juhudi zinazochukuliwa na serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo kupambana na ungojwa huo.

Alilitaka shirika hilo katika kutekeleza mradi huo kuziwezesha serikali za mitaa ili nazo zishiriki katika kutoa elimu katika ngazi za shehia ili wananchi waweze kujilinda.

Naye Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Amref Health Africa, Florence Temu, alisema mradi huo wa afya kamilifu unalenga kuongeza idadi ya watu wanaojijua kuwa wanaishi na VVU na Ukimwi wanapata huduma za upimaji wa VVU na ushauri, matunzo na matibabu ya kufubaza virusi ili kuhakikisha kwamba vinafubazwa.

“Hadi kufikia mwisho wa mradi tunalenga kuhakikisha kwamba watu wote wanaoishi na VVU na Ukimwi watakua wanajua hali zao na wanapata matibabu,” alisema.

Kwa upande wake, Meneja wa mradi huo, Edwin Kilimba, alisema kwa zaidi ya miaka 30 shirika la Amref Health Afrika limekuwa likishirikiana na serikali ya Tanzania na wadau wengine kuimarisha mifumo ya afya nchini ili kuondoa changamoto zinazochochea kurudisha nyuma maendeleo.

Article first published on https://www.ippmedia.com/sw/habari/mkakati-mpya-kumaliza-ukimwi-2030

Amref Health Africa

Amref Health Africa teams up with African communities to create lasting health change.

Recent Posts

Western Kenya Deworms More Than 5 Million People in an Ambitious Bid to Eliminate Intestinal Worms and Bilharzia

In four counties of western Kenya, a silent but intense battle is being fought against…

2 days ago

Promoting Indigenous Knowledge for Climate Action

In 1986, Mzee Lepoo watched his father save their village from devastating floods. By observing…

4 days ago

Site Inspection for PSA Oxygen-Generating Plants in Six Hospitals

Amref Health Africa in Kenya in partnership with Global Fund has successfully constructed and carried…

2 weeks ago

Call for Nominations: AHAIC 2025 Women in Global Health Awards to Honour Africa’s Most Inspiring Changemakers

Nairobi, 7 February 2025: In the lead-up to International Women's Day 2025, the Africa Health Agenda International…

2 weeks ago

At the World Economic Forum, UNFPA’s private sector champions commit to workplace reproductive health policies reaching more than 300,000 employees

DAVOS, Switzerland – At this year’s World Economic Forum, UNFPA and private sector partners Amref, Bayer,…

4 weeks ago

Financing the Future: Strengthening Health Systems Amidst the Climate and Health Crisis

Climate change is projected to cause approximately 250,000 additional deaths annually between 2030 and 2050, with undernutrition,…

1 month ago