Categories: News

Mkakati mpya kumaliza Ukimwi 2030

Uzinduzi wa mradi huo ujulikanao Afya kamilifu ulifanyika  Maruhubi Mjini Zanzibar na kuzinduliwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Zanzibar, Asha Abdallah Ali.

Akizungumza baada ya kuzindua mradi huo, alisema Serikali itaendelea kuunga mkono jitihada za shirika hilo lenye lengo la kupambana na Ukimwi Zanzibar.

Aliliomba shirika hilo kuongeza nguvu zaidi katika makundi maalum kwa kuwa bado maambukizi ni makubwa kulinganisha na watu wa kawasaidia.

Aliyataja makundi hayo ni watumiaji wa dawa za kulevya wanaojidunga sindano, wanawake wanaofanya biashara ya ngono na wanaume wanaofanya mapenzi ya jinsia moja.

Aidha, alisema Zanzibar ina asilimia moja ya kiwango cha maambukizi na hiyo inatokana na juhudi zinazochukuliwa na serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo kupambana na ungojwa huo.

Alilitaka shirika hilo katika kutekeleza mradi huo kuziwezesha serikali za mitaa ili nazo zishiriki katika kutoa elimu katika ngazi za shehia ili wananchi waweze kujilinda.

Naye Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Amref Health Africa, Florence Temu, alisema mradi huo wa afya kamilifu unalenga kuongeza idadi ya watu wanaojijua kuwa wanaishi na VVU na Ukimwi wanapata huduma za upimaji wa VVU na ushauri, matunzo na matibabu ya kufubaza virusi ili kuhakikisha kwamba vinafubazwa.

“Hadi kufikia mwisho wa mradi tunalenga kuhakikisha kwamba watu wote wanaoishi na VVU na Ukimwi watakua wanajua hali zao na wanapata matibabu,” alisema.

Kwa upande wake, Meneja wa mradi huo, Edwin Kilimba, alisema kwa zaidi ya miaka 30 shirika la Amref Health Afrika limekuwa likishirikiana na serikali ya Tanzania na wadau wengine kuimarisha mifumo ya afya nchini ili kuondoa changamoto zinazochochea kurudisha nyuma maendeleo.

Article first published on https://www.ippmedia.com/sw/habari/mkakati-mpya-kumaliza-ukimwi-2030

Amref Health Africa

Amref Health Africa teams up with African communities to create lasting health change.

Recent Posts

REACH-OUT Project Stakeholders in Busia County Co-Create Evidence-Informed Solutions to Strengthen Childhood Immunisation

The REACH-OUT Project held a dynamic two-day co-creation workshop in Busia County, bringing together National…

10 hours ago

The Power of Connection: Reflections from the 2026 International SBCC Summit

In June, I travelled to Panama City to represent Amref Health Africa at the 2026 International…

13 hours ago

REACH-OUT Advances Digital Innovation to Strengthen Immunisation Microplanning in Kenya

Despite significant progress in immunisation, many children still miss out on life-saving vaccines. Health systems…

15 hours ago

Making Safe Care Possible, One Drop at a Time

"How do you deliver a baby without water?"  For Laurence Erongat, a Nursing Officer at Lopiding Hospital…

3 days ago

AHAIC’s Flags of Unity Wins Silver at the Prestigious 2026 Creative Circle Awards

The Africa Health Agenda International Conference (AHAIC) continues to strengthen its position as one of Africa's most…

1 week ago

I Will Cross The Waters For You: The Weight on Emmanuel Malama, Zambia’s Community Health Worker

In this parts its to understand that for many families, the first line of care…

2 weeks ago