Categories: News

Mkakati mpya kumaliza Ukimwi 2030

Uzinduzi wa mradi huo ujulikanao Afya kamilifu ulifanyika  Maruhubi Mjini Zanzibar na kuzinduliwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Zanzibar, Asha Abdallah Ali.

Akizungumza baada ya kuzindua mradi huo, alisema Serikali itaendelea kuunga mkono jitihada za shirika hilo lenye lengo la kupambana na Ukimwi Zanzibar.

Aliliomba shirika hilo kuongeza nguvu zaidi katika makundi maalum kwa kuwa bado maambukizi ni makubwa kulinganisha na watu wa kawasaidia.

Aliyataja makundi hayo ni watumiaji wa dawa za kulevya wanaojidunga sindano, wanawake wanaofanya biashara ya ngono na wanaume wanaofanya mapenzi ya jinsia moja.

Aidha, alisema Zanzibar ina asilimia moja ya kiwango cha maambukizi na hiyo inatokana na juhudi zinazochukuliwa na serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo kupambana na ungojwa huo.

Alilitaka shirika hilo katika kutekeleza mradi huo kuziwezesha serikali za mitaa ili nazo zishiriki katika kutoa elimu katika ngazi za shehia ili wananchi waweze kujilinda.

Naye Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Amref Health Africa, Florence Temu, alisema mradi huo wa afya kamilifu unalenga kuongeza idadi ya watu wanaojijua kuwa wanaishi na VVU na Ukimwi wanapata huduma za upimaji wa VVU na ushauri, matunzo na matibabu ya kufubaza virusi ili kuhakikisha kwamba vinafubazwa.

“Hadi kufikia mwisho wa mradi tunalenga kuhakikisha kwamba watu wote wanaoishi na VVU na Ukimwi watakua wanajua hali zao na wanapata matibabu,” alisema.

Kwa upande wake, Meneja wa mradi huo, Edwin Kilimba, alisema kwa zaidi ya miaka 30 shirika la Amref Health Afrika limekuwa likishirikiana na serikali ya Tanzania na wadau wengine kuimarisha mifumo ya afya nchini ili kuondoa changamoto zinazochochea kurudisha nyuma maendeleo.

Article first published on https://www.ippmedia.com/sw/habari/mkakati-mpya-kumaliza-ukimwi-2030

Amref Health Africa

Amref Health Africa teams up with African communities to create lasting health change.

Recent Posts

Harvesting Hope: Transforming Health of Communities through Kitchen Gardening in South Suda

Step into the heart of South Sudan, where a powerful movement is taking root through…

12 hours ago

Uzazi Salama Programme Launches in Kilifi County

The KES 225 Million investment aims to impact 500,000 lives by supporting reproductive, maternal, neonatal,…

4 days ago

African campaigner calls for targeted interventions to eliminate malaria

NAIROBI, April 25 (Xinhua) -- The goal of eliminating malaria in Africa by 2030 can…

4 days ago

Does Africa need a rethink on tackling violent extremism?

African leaders meeting at a security summit in Nigeria say the continent needs a new…

4 days ago

Saving Lives through Better Malaria Diagnosis

Malaria remains a major public health problem in tropical regions of the world. Despite being…

5 days ago

Incentivizing Non-monetary Volunteering: Improving community involvement with In-kind motivation in public health services.

Just before the Vaccination Action Network (VAN), the Infectious Diseases Institute (IDI) set out to…

6 days ago