News

AMREF kushirikiana na jamii ya kimaasai kutunga sheria ya ukeketeji

SHIRIKA lisilo la kiserikali AMREF wakishirikiana na jamii ya kabila la kimasai (Laigwanani) kutoka Wilaya ya Handeni na Kilindi wamekubaliana kutunga sheria mpya za kimila kuhusiana na ukeketaji kwa watoto wa kike huku sheria kubwa ikiwa ni kutengwa na jamii.

Mkakati huo umepangwa wakati wa kikao cha kujadili jinsi ya kupinga na kuzuia ukeketaji  kilichoandaliwa na Shirika la AMREF, ambapo wamesema wanatunga sheria hizo sambamba na kutoa elimu, hivyo atakaebainika kufanya vitendo hivyo adhabu itachukuliwa dhidi yake.

William Tangono, ambaye ni mmoja wa Laigwanani kutoka kabila hilo amesema wanaweka sheria za kimila ili kupinga na kuzuia ukeketaji na pia kuungana na serikali kutokomeza suala hili.

“Sisi kama watetezi wa wananchi Malaigwanani lazima tuweke sheria za kimila kwa sababu hata serikali inapinga marufuku, hivyo na sisi tukiingiza sheria za kimila itasaidia kupunguza au kutokomeza kabisa” Amesema Tangono

Naye Simon Ngosha, mmoja wa waliohudhuria katika kikao hicho amesema “Tukiweka sheria za kimila itasaidia mtu kuwa na hofu kutokana na laana za jamii yake kwa sababu watu wengi huogopa sana laana kuliko kitu chochote”Amesema.

Rehema Kamando, mdau wa kupinga ukeketaji amesema elimu itolewe hasa kwa wazee wa kabila hilo kwa kuwa ndio wahusika wakuu kwani wao ndio wanakeketa watoto wakiwa wadogo kwa siri pindi wazaliwapo hali ambayo hupelekea baba wa mototo kutojua.

Meneja Mradi AMREF, Dkt. Jane Sempeho, amesema wameamua kuanzisha mradi huo mdogo kwa ajili ya kuhamasisha jamii zinazohusika na masuala ya ukeketaji ili waweze kuacha kwa sababu ni kinyume cha haki za binadamu.

Content retrieved from: https://ippmedia.com/sw/habari/amref-kushirikiana-na-jamii-ya-kimaasai-kutunga-sheria-ya-ukeketeji.

Amref Health Africa

Amref Health Africa teams up with African communities to create lasting health change.

Recent Posts

Western Kenya Deworms More Than 5 Million People in an Ambitious Bid to Eliminate Intestinal Worms and Bilharzia

In four counties of western Kenya, a silent but intense battle is being fought against…

2 days ago

Promoting Indigenous Knowledge for Climate Action

In 1986, Mzee Lepoo watched his father save their village from devastating floods. By observing…

4 days ago

Site Inspection for PSA Oxygen-Generating Plants in Six Hospitals

Amref Health Africa in Kenya in partnership with Global Fund has successfully constructed and carried…

2 weeks ago

Call for Nominations: AHAIC 2025 Women in Global Health Awards to Honour Africa’s Most Inspiring Changemakers

Nairobi, 7 February 2025: In the lead-up to International Women's Day 2025, the Africa Health Agenda International…

2 weeks ago

At the World Economic Forum, UNFPA’s private sector champions commit to workplace reproductive health policies reaching more than 300,000 employees

DAVOS, Switzerland – At this year’s World Economic Forum, UNFPA and private sector partners Amref, Bayer,…

1 month ago

Financing the Future: Strengthening Health Systems Amidst the Climate and Health Crisis

Climate change is projected to cause approximately 250,000 additional deaths annually between 2030 and 2050, with undernutrition,…

1 month ago