News

AMREF kushirikiana na jamii ya kimaasai kutunga sheria ya ukeketeji

SHIRIKA lisilo la kiserikali AMREF wakishirikiana na jamii ya kabila la kimasai (Laigwanani) kutoka Wilaya ya Handeni na Kilindi wamekubaliana kutunga sheria mpya za kimila kuhusiana na ukeketaji kwa watoto wa kike huku sheria kubwa ikiwa ni kutengwa na jamii.

Mkakati huo umepangwa wakati wa kikao cha kujadili jinsi ya kupinga na kuzuia ukeketaji  kilichoandaliwa na Shirika la AMREF, ambapo wamesema wanatunga sheria hizo sambamba na kutoa elimu, hivyo atakaebainika kufanya vitendo hivyo adhabu itachukuliwa dhidi yake.

William Tangono, ambaye ni mmoja wa Laigwanani kutoka kabila hilo amesema wanaweka sheria za kimila ili kupinga na kuzuia ukeketaji na pia kuungana na serikali kutokomeza suala hili.

“Sisi kama watetezi wa wananchi Malaigwanani lazima tuweke sheria za kimila kwa sababu hata serikali inapinga marufuku, hivyo na sisi tukiingiza sheria za kimila itasaidia kupunguza au kutokomeza kabisa” Amesema Tangono

Naye Simon Ngosha, mmoja wa waliohudhuria katika kikao hicho amesema “Tukiweka sheria za kimila itasaidia mtu kuwa na hofu kutokana na laana za jamii yake kwa sababu watu wengi huogopa sana laana kuliko kitu chochote”Amesema.

Rehema Kamando, mdau wa kupinga ukeketaji amesema elimu itolewe hasa kwa wazee wa kabila hilo kwa kuwa ndio wahusika wakuu kwani wao ndio wanakeketa watoto wakiwa wadogo kwa siri pindi wazaliwapo hali ambayo hupelekea baba wa mototo kutojua.

Meneja Mradi AMREF, Dkt. Jane Sempeho, amesema wameamua kuanzisha mradi huo mdogo kwa ajili ya kuhamasisha jamii zinazohusika na masuala ya ukeketaji ili waweze kuacha kwa sababu ni kinyume cha haki za binadamu.

Content retrieved from: https://ippmedia.com/sw/habari/amref-kushirikiana-na-jamii-ya-kimaasai-kutunga-sheria-ya-ukeketeji.

Amref Health Africa

Amref Health Africa teams up with African communities to create lasting health change.

Recent Posts

Making Safe Care Possible, One Drop at a Time

"How do you deliver a baby without water?"  For Laurence Erongat, a Nursing Officer at Lopiding Hospital…

3 hours ago

AHAIC’s Flags of Unity Wins Silver at the Prestigious 2026 Creative Circle Awards

The Africa Health Agenda International Conference (AHAIC) continues to strengthen its position as one of Africa's most…

6 days ago

I Will Cross The Waters For You: The Weight on Emmanuel Malama, Zambia’s Community Health Worker

In this parts its to understand that for many families, the first line of care…

2 weeks ago

How climate change is redrawing Africa’s malaria map

The gains made in reducing malaria cases around the world are being put in jeopardy…

2 weeks ago

Empowering Health Workers to Reach Zero-Dose Children in Underserved Communities in Busia County, Kenya

Vaccines are among the most effective public health tools, preventing serious illnesses, disabilities, and deaths…

2 weeks ago

Kenyans Protest Proposed US Ebola Facility

BBC World Service BBC World Service examines the debate surrounding the proposed US Ebola quarantine…

3 weeks ago