News

AMREF kushirikiana na jamii ya kimaasai kutunga sheria ya ukeketeji

SHIRIKA lisilo la kiserikali AMREF wakishirikiana na jamii ya kabila la kimasai (Laigwanani) kutoka Wilaya ya Handeni na Kilindi wamekubaliana kutunga sheria mpya za kimila kuhusiana na ukeketaji kwa watoto wa kike huku sheria kubwa ikiwa ni kutengwa na jamii.

Mkakati huo umepangwa wakati wa kikao cha kujadili jinsi ya kupinga na kuzuia ukeketaji  kilichoandaliwa na Shirika la AMREF, ambapo wamesema wanatunga sheria hizo sambamba na kutoa elimu, hivyo atakaebainika kufanya vitendo hivyo adhabu itachukuliwa dhidi yake.

William Tangono, ambaye ni mmoja wa Laigwanani kutoka kabila hilo amesema wanaweka sheria za kimila ili kupinga na kuzuia ukeketaji na pia kuungana na serikali kutokomeza suala hili.

“Sisi kama watetezi wa wananchi Malaigwanani lazima tuweke sheria za kimila kwa sababu hata serikali inapinga marufuku, hivyo na sisi tukiingiza sheria za kimila itasaidia kupunguza au kutokomeza kabisa” Amesema Tangono

Naye Simon Ngosha, mmoja wa waliohudhuria katika kikao hicho amesema “Tukiweka sheria za kimila itasaidia mtu kuwa na hofu kutokana na laana za jamii yake kwa sababu watu wengi huogopa sana laana kuliko kitu chochote”Amesema.

Rehema Kamando, mdau wa kupinga ukeketaji amesema elimu itolewe hasa kwa wazee wa kabila hilo kwa kuwa ndio wahusika wakuu kwani wao ndio wanakeketa watoto wakiwa wadogo kwa siri pindi wazaliwapo hali ambayo hupelekea baba wa mototo kutojua.

Meneja Mradi AMREF, Dkt. Jane Sempeho, amesema wameamua kuanzisha mradi huo mdogo kwa ajili ya kuhamasisha jamii zinazohusika na masuala ya ukeketaji ili waweze kuacha kwa sababu ni kinyume cha haki za binadamu.

Content retrieved from: https://ippmedia.com/sw/habari/amref-kushirikiana-na-jamii-ya-kimaasai-kutunga-sheria-ya-ukeketeji.

Amref Health Africa

Amref Health Africa teams up with African communities to create lasting health change.

Recent Posts

Uzazi Salama Programme Launches in Kilifi County

The KES 225 Million investment aims to impact 500,000 lives by supporting reproductive, maternal, neonatal,…

1 day ago

African campaigner calls for targeted interventions to eliminate malaria

NAIROBI, April 25 (Xinhua) -- The goal of eliminating malaria in Africa by 2030 can…

1 day ago

Does Africa need a rethink on tackling violent extremism?

African leaders meeting at a security summit in Nigeria say the continent needs a new…

2 days ago

Saving Lives through Better Malaria Diagnosis

Malaria remains a major public health problem in tropical regions of the world. Despite being…

2 days ago

Incentivizing Non-monetary Volunteering: Improving community involvement with In-kind motivation in public health services.

Just before the Vaccination Action Network (VAN), the Infectious Diseases Institute (IDI) set out to…

3 days ago

Amref Health Africa Achieves SWA Partnership Commitment through first-ever Pan-African Common Position on Climate and Health.

Amref Health Africa, the leading health NGO in Africa, has successfully achieved its Mutual Accountability Mechanism…

1 week ago