News

AMREF kushirikiana na jamii ya kimaasai kutunga sheria ya ukeketeji

SHIRIKA lisilo la kiserikali AMREF wakishirikiana na jamii ya kabila la kimasai (Laigwanani) kutoka Wilaya ya Handeni na Kilindi wamekubaliana kutunga sheria mpya za kimila kuhusiana na ukeketaji kwa watoto wa kike huku sheria kubwa ikiwa ni kutengwa na jamii.

Mkakati huo umepangwa wakati wa kikao cha kujadili jinsi ya kupinga na kuzuia ukeketaji  kilichoandaliwa na Shirika la AMREF, ambapo wamesema wanatunga sheria hizo sambamba na kutoa elimu, hivyo atakaebainika kufanya vitendo hivyo adhabu itachukuliwa dhidi yake.

William Tangono, ambaye ni mmoja wa Laigwanani kutoka kabila hilo amesema wanaweka sheria za kimila ili kupinga na kuzuia ukeketaji na pia kuungana na serikali kutokomeza suala hili.

“Sisi kama watetezi wa wananchi Malaigwanani lazima tuweke sheria za kimila kwa sababu hata serikali inapinga marufuku, hivyo na sisi tukiingiza sheria za kimila itasaidia kupunguza au kutokomeza kabisa” Amesema Tangono

Naye Simon Ngosha, mmoja wa waliohudhuria katika kikao hicho amesema “Tukiweka sheria za kimila itasaidia mtu kuwa na hofu kutokana na laana za jamii yake kwa sababu watu wengi huogopa sana laana kuliko kitu chochote”Amesema.

Rehema Kamando, mdau wa kupinga ukeketaji amesema elimu itolewe hasa kwa wazee wa kabila hilo kwa kuwa ndio wahusika wakuu kwani wao ndio wanakeketa watoto wakiwa wadogo kwa siri pindi wazaliwapo hali ambayo hupelekea baba wa mototo kutojua.

Meneja Mradi AMREF, Dkt. Jane Sempeho, amesema wameamua kuanzisha mradi huo mdogo kwa ajili ya kuhamasisha jamii zinazohusika na masuala ya ukeketaji ili waweze kuacha kwa sababu ni kinyume cha haki za binadamu.

Content retrieved from: https://ippmedia.com/sw/habari/amref-kushirikiana-na-jamii-ya-kimaasai-kutunga-sheria-ya-ukeketeji.

Amref Health Africa

Amref Health Africa teams up with African communities to create lasting health change.

Recent Posts

Let’s recommit to strategies for a malaria-free, equitable world by 2030

Today provides an opportunity for the global community to reflect on the progress made in…

2 days ago

How innovation and Collaboration will transform Turkana Children’s future

Kenya’s largest county by landmass sprawls across the north-western corner, enveloping nearly 77,000 square kilometres…

2 days ago

Harvesting Hope: Transforming Health of Communities through Kitchen Gardening in South Suda

Step into the heart of South Sudan, where a powerful movement is taking root through…

5 days ago

Uzazi Salama Programme Launches in Kilifi County

The KES 225 Million investment aims to impact 500,000 lives by supporting reproductive, maternal, neonatal,…

1 week ago

African campaigner calls for targeted interventions to eliminate malaria

NAIROBI, April 25 (Xinhua) -- The goal of eliminating malaria in Africa by 2030 can…

1 week ago

Does Africa need a rethink on tackling violent extremism?

African leaders meeting at a security summit in Nigeria say the continent needs a new…

1 week ago