Categories: News

Tamasha la Jenga Jirani

Janga la Corona limeathiri watu wengi ulimwenguni kote kiasi cha kutoweza kujipatia mahitaji ya msingi kama vile chakula.

Hata hivyo kuna wale ambao wanajali watu kama hao kama vile wakfu wa “Jackson” na kampuni ya burudani inayojulikana kama “Kubamba Krew”.

Asasi hizo mbili zimungana na kuanzisha mpango unaojulikana kama “Jenga Jirani” kwa lengo la kuchangisha pesa za kusaidia walio na mahitaji baada ya kuathiriwa na janga la Corona.

Na sasa wameandaa tamasha ambalo litapeperushwa kwa mitandao ya kijamii wikendi ijayo ambalo linalenga kuchangisha milioni 100.

Jackson Jonathan ambaye ni mwanzilishi wa wakfu wa Jackson alihimiza wakenya wajitolee kusaidia wenzao huku akiahidi kwamba kutakuwa na uwazi kuhusu matumizi ya fedha zitakazokusanywa.

Alisema wameshirikiana na shirika la AMREF ambapo pesa zote zitakazokusanywa zitawekwa kwenye akaunti ya AMREF kisha waunde kamati ya ushauri kuhusu njia mwafaka ya kutumia pesa hizo kugusa maisha ya wakenya walio na mahitaji.

Wanamuziki kadhaa wa hadhi ya juu nchini Kenya watatumbuiza kwenye tamasha hilo na wanajumuisha Nyashinski, Khaligraph Jones, Samidoh, Juliani. Mercy Masika na Erick Wainaina.

Wachekeshaji kama vile Eric Omondi na Mc Jessy pia watakuwa pale kutumbuiza.

Tamasha hilo litakuwa la tarehe saba na tarehe nane mwezi huu wa Novemba mwaka 2020 na unaweza kufuatilia matukio kwenye tovuti ya Jenga Jirani.

Article first published on radiotaifa.co.ke

Amref Health Africa

Amref Health Africa teams up with African communities to create lasting health change.

Recent Posts

Western Kenya Deworms More Than 5 Million People in an Ambitious Bid to Eliminate Intestinal Worms and Bilharzia

In four counties of western Kenya, a silent but intense battle is being fought against…

2 days ago

Promoting Indigenous Knowledge for Climate Action

In 1986, Mzee Lepoo watched his father save their village from devastating floods. By observing…

4 days ago

Site Inspection for PSA Oxygen-Generating Plants in Six Hospitals

Amref Health Africa in Kenya in partnership with Global Fund has successfully constructed and carried…

2 weeks ago

Call for Nominations: AHAIC 2025 Women in Global Health Awards to Honour Africa’s Most Inspiring Changemakers

Nairobi, 7 February 2025: In the lead-up to International Women's Day 2025, the Africa Health Agenda International…

2 weeks ago

At the World Economic Forum, UNFPA’s private sector champions commit to workplace reproductive health policies reaching more than 300,000 employees

DAVOS, Switzerland – At this year’s World Economic Forum, UNFPA and private sector partners Amref, Bayer,…

1 month ago

Financing the Future: Strengthening Health Systems Amidst the Climate and Health Crisis

Climate change is projected to cause approximately 250,000 additional deaths annually between 2030 and 2050, with undernutrition,…

1 month ago