Categories: News

Tamasha la Jenga Jirani

Janga la Corona limeathiri watu wengi ulimwenguni kote kiasi cha kutoweza kujipatia mahitaji ya msingi kama vile chakula.

Hata hivyo kuna wale ambao wanajali watu kama hao kama vile wakfu wa “Jackson” na kampuni ya burudani inayojulikana kama “Kubamba Krew”.

Asasi hizo mbili zimungana na kuanzisha mpango unaojulikana kama “Jenga Jirani” kwa lengo la kuchangisha pesa za kusaidia walio na mahitaji baada ya kuathiriwa na janga la Corona.

Na sasa wameandaa tamasha ambalo litapeperushwa kwa mitandao ya kijamii wikendi ijayo ambalo linalenga kuchangisha milioni 100.

Jackson Jonathan ambaye ni mwanzilishi wa wakfu wa Jackson alihimiza wakenya wajitolee kusaidia wenzao huku akiahidi kwamba kutakuwa na uwazi kuhusu matumizi ya fedha zitakazokusanywa.

Alisema wameshirikiana na shirika la AMREF ambapo pesa zote zitakazokusanywa zitawekwa kwenye akaunti ya AMREF kisha waunde kamati ya ushauri kuhusu njia mwafaka ya kutumia pesa hizo kugusa maisha ya wakenya walio na mahitaji.

Wanamuziki kadhaa wa hadhi ya juu nchini Kenya watatumbuiza kwenye tamasha hilo na wanajumuisha Nyashinski, Khaligraph Jones, Samidoh, Juliani. Mercy Masika na Erick Wainaina.

Wachekeshaji kama vile Eric Omondi na Mc Jessy pia watakuwa pale kutumbuiza.

Tamasha hilo litakuwa la tarehe saba na tarehe nane mwezi huu wa Novemba mwaka 2020 na unaweza kufuatilia matukio kwenye tovuti ya Jenga Jirani.

Article first published on radiotaifa.co.ke

Amref Health Africa

Amref Health Africa teams up with African communities to create lasting health change.

Recent Posts

Making Safe Care Possible, One Drop at a Time

"How do you deliver a baby without water?"  For Laurence Erongat, a Nursing Officer at Lopiding Hospital…

7 hours ago

AHAIC’s Flags of Unity Wins Silver at the Prestigious 2026 Creative Circle Awards

The Africa Health Agenda International Conference (AHAIC) continues to strengthen its position as one of Africa's most…

6 days ago

I Will Cross The Waters For You: The Weight on Emmanuel Malama, Zambia’s Community Health Worker

In this parts its to understand that for many families, the first line of care…

2 weeks ago

How climate change is redrawing Africa’s malaria map

The gains made in reducing malaria cases around the world are being put in jeopardy…

2 weeks ago

Empowering Health Workers to Reach Zero-Dose Children in Underserved Communities in Busia County, Kenya

Vaccines are among the most effective public health tools, preventing serious illnesses, disabilities, and deaths…

2 weeks ago

Kenyans Protest Proposed US Ebola Facility

BBC World Service BBC World Service examines the debate surrounding the proposed US Ebola quarantine…

3 weeks ago