Categories: News

Amref yapunguza wenye VVU wanaopotea kwenye matibabu Simiyu

Shirika la Amref Health Africa limesema kuwa kupitia mradi wake wa Afya Kamilifu ambao unatekelezwa katika mikoa ya Simiyu, Tanga pamoja na Zanzibar limefanikiwa kupunguza idadi kubwa ya watu ambao wanaishi na VVU kupotea katika matibabu.

Kwa Mkoa wa Simiyu, Shirika hilo limeeleza kuwa katika halmashauri ya mji wa Bariadi kwa kushirikiana na serikali wamefanikiwa kupunguza kiwango cha wenye VVU wanaopotea kwenye matatibabu kutoka 472 hadi 146 kwa kipindi cha miezi sita ndani ya mwaka huu.

Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi wa mradi huo, Dk. Edwine Kilimba kutoka Amref wakati akiwasilisha taarifa ya kazi zinazotekelezwa na Shirika hilo chini ya Mradi huo kwenye kikao kilichowakutanisha wadau wa sekta ya Afya mkoa wa Simiyu.

Dk. Kilimba amesema kuwa licha ya jitihada hizo za kupunguza watu wanaopotea, bado changamoto ipo ya baadhi ya wenye VVU kutoweka katika matibabu huku akieleza kuwa sababu kubwa ni kushindwa kutimiza wajibu kwa baadhi ya watumishi wa Afya.

Amesema kuwa kupitia mradi huo, Amref imelenga kufikia asilimia 95 ya watu wenye VVU wanajitambua kwa kupima, kufikia asilimia 95 ya waliojitambua kuwa kwenye dawa, pamoja na kufikia asilimia 95 wanaotumia dawa waweze kufubaza Virusi.

Aidha, amesema kuwa toka mwezi Oktaba 2020 hadi Machi 2021, wameongeza kiwango cha upimaji kwa watoto wadogo kutoka asilimia 39 hadi asilimia 86 mpaka sasa huku kiwango cha wenye VVU kufubaza virusi kikiongezeka.

“Katika eneo la kufubuza virusi kwa wenye maambukizi, tumefanikiwa kwa kiwango kikubwa, kwani kwenye maeneo yote ambayo mradi upo, Simiyu, Tanga, Zanzibar, wenye VVU wamepunguza kiwango cha kuambukiza (kufubaza virusi) kwa asilimia 90,” amesema Dk. Kilimba.

Awali, akizungumzia hali ya huduma za Afya Mkoani humo, mganga Mkuu wa Mkoa, Dk. Boniphace Marwa amesema mkoa umeendelea kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto wadogo.

Dk. Marwa ameeleza kuwa vifo ambavyo vimeendelea kutokea, vinasababishwa kwa kiwango kikubwa na uzembe wa watumishi kutokana na kushindwa kutimiza wajibu wao ipasavyo.

Akifunga kikao hicho Mkuu wa mkoa huo, David Kafulila amezita kamati za Afya za wilaya kuhakikisha zinatekeleza wajibu wao ipasavyo kwa kuhakikisha huduma za Afya zinatolewa kikamilifu kwa wananchi.

This article was first published on Gazeti la Mtanzania.

Amref Health Africa

Amref Health Africa teams up with African communities to create lasting health change.

View Comments

  • Ni kazi nzuri Sana hongereni na poleni kwa kazi kubwa mnayofanya.mi pia nimefanya kazi hiyo na ninaielewa changamoto zake

Recent Posts

REACH-OUT Project Stakeholders in Busia County Co-Create Evidence-Informed Solutions to Strengthen Childhood Immunisation

The REACH-OUT Project held a dynamic two-day co-creation workshop in Busia County, bringing together National…

2 days ago

The Power of Connection: Reflections from the 2026 International SBCC Summit

In June, I travelled to Panama City to represent Amref Health Africa at the 2026 International…

2 days ago

REACH-OUT Advances Digital Innovation to Strengthen Immunisation Microplanning in Kenya

Despite significant progress in immunisation, many children still miss out on life-saving vaccines. Health systems…

3 days ago

Making Safe Care Possible, One Drop at a Time

"How do you deliver a baby without water?"  For Laurence Erongat, a Nursing Officer at Lopiding Hospital…

5 days ago

AHAIC’s Flags of Unity Wins Silver at the Prestigious 2026 Creative Circle Awards

The Africa Health Agenda International Conference (AHAIC) continues to strengthen its position as one of Africa's most…

1 week ago

I Will Cross The Waters For You: The Weight on Emmanuel Malama, Zambia’s Community Health Worker

In this parts its to understand that for many families, the first line of care…

3 weeks ago