NAIBU WAZIRI WA AFYA DKT. MOLLEL AKABIDHI VYANDARUA KWA WANAWAKE SHINYANGA MJINI
Katika kuadhimisha siku ya Malaria Duniani, Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel ameungana na mwenyeji wake Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe Pascal Patrobas Katambi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini kugawa vyandarua kwa wanawake zaidi ya 400 pamoja na kufikia makundi mbalimbali ya wananchi katika jamii ndani ya Manispaa ya Shinyanga.
Dkt. Mollel ameipongeza Taasisi ya Doris Mollel kwa kushirikiana na Amref kuja na mkakati huo wa kuwafikia wananchi moja kwa moja na kuweza kutoa misaada mbalimbali inayogusa maisha ya Watanzania.
Katika Warsha iliyohudhuriwa na wanawake zaidi ya 400, Dkt. Mollel amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imelenga kuboresha huduma za uzazi, mama na mtoto na kuhakikisha jamii inapata elimu ya kutosha na kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.
“Asante wakina mama mliokuja hapa kupata elimu ili mkatusaidie kuelimisha wengine na kupunguza vifo vya akina mama na watoto” amepongeza Dkt. Mollel
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Doris Mollel Bi. Doris Mollel amesema kuwa lengo la warsha hiyo ni kutoa elimu ya ugonjwa malaria na namna ya kujikinga pamoja na kuhamasisha wanawake kujitokeza kupata chanjo ya UVIKO-19 ili waweze kujikinga janga hili kubwa la korona, tunaliona linaisha ila bado ugonjwa upo.
“Zoezi limefanyika katika mikoa mitatu kwa kushirikiana na Amref kwa mikoa ya Simiyu, Kagera na Shinyanga na tunaishukuru Serikali kwa kutuwekea mazingira wezeshi sisi taasisi binafsi kuweza kufanya kazi na kutoa mchango wetu ndani ya jamii” amesema Doris Mollel.
Article first published on https://issamichuzi.blogspot.com/2022/04/naibu-waziri-wa-afya-dkt-mollel.html
In four counties of western Kenya, a silent but intense battle is being fought against…
In 1986, Mzee Lepoo watched his father save their village from devastating floods. By observing…
Amref Health Africa in Kenya in partnership with Global Fund has successfully constructed and carried…
Nairobi, 7 February 2025: In the lead-up to International Women's Day 2025, the Africa Health Agenda International…
DAVOS, Switzerland – At this year’s World Economic Forum, UNFPA and private sector partners Amref, Bayer,…
Climate change is projected to cause approximately 250,000 additional deaths annually between 2030 and 2050, with undernutrition,…