News

NAIBU WAZIRI WA AFYA DKT. MOLLEL AKABIDHI VYANDARUA KWA WANAWAKE SHINYANGA MJINI

Katika kuadhimisha siku ya Malaria Duniani, Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel ameungana na mwenyeji wake Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe Pascal Patrobas Katambi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini kugawa vyandarua kwa wanawake zaidi ya 400 pamoja na kufikia makundi mbalimbali ya wananchi katika jamii ndani ya Manispaa ya Shinyanga.

Dkt. Mollel ameipongeza Taasisi ya Doris Mollel kwa kushirikiana na Amref kuja na mkakati huo wa kuwafikia wananchi moja kwa moja na kuweza kutoa misaada mbalimbali inayogusa maisha ya Watanzania.

Naibu waziri wa afya dkt. Mollel akabithi vyandarua kwa wanawake Shinyanga mjini

Katika Warsha iliyohudhuriwa na wanawake zaidi ya 400, Dkt. Mollel amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imelenga kuboresha huduma za uzazi, mama na mtoto na kuhakikisha jamii inapata elimu ya kutosha na kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.

“Asante wakina mama mliokuja hapa kupata elimu ili mkatusaidie kuelimisha wengine na kupunguza vifo vya akina mama na watoto” amepongeza Dkt. Mollel

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Doris Mollel Bi. Doris Mollel amesema kuwa lengo la warsha hiyo ni kutoa elimu ya ugonjwa malaria na namna ya kujikinga pamoja na kuhamasisha wanawake kujitokeza kupata chanjo ya UVIKO-19 ili waweze kujikinga janga hili kubwa la korona, tunaliona linaisha ila bado ugonjwa upo.

“Zoezi limefanyika katika mikoa mitatu kwa kushirikiana na Amref kwa mikoa ya Simiyu, Kagera na Shinyanga na tunaishukuru Serikali kwa kutuwekea mazingira wezeshi sisi taasisi binafsi kuweza kufanya kazi na kutoa mchango wetu ndani ya jamii” amesema Doris Mollel.

Article first published on https://issamichuzi.blogspot.com/2022/04/naibu-waziri-wa-afya-dkt-mollel.html

Amref Health Africa

Amref Health Africa teams up with African communities to create lasting health change.

Recent Posts

From Crisis to Opportunity: Secure Africa’s Health Future Now

Authors: Boniface Mbuthia, Rahul S Reddy Kadarpeta, David Olpengs, Charlotte Muheki As the world marks…

3 days ago

A water investment that is powering entrepreneurship and transforming Maasai land

Growing up in Maasai land, Sylvia Seleon always imagined a future where her community no longer struggled…

3 days ago

Amref Health Africa and Qatar Fund for Development Partner to transform urban health for over 225,000 Kenyans

Doha, Qatar – [6th December, 2025] – In a move set to redefine urban health standards in East Africa, Amref Health Africa today…

6 days ago

Building the Next Generation of Health Leaders in Ethiopia

In a region where health workers often carry the weight of entire communities on their…

6 days ago

The Rise of a Youth Advocate Who Is Helping Strengthen Ethiopia’s Immunisation System

At just 24 years old, Tsedenia Tadele carries a story that reflects the lived experiences…

2 weeks ago

A Mother’s Hope Restored as Conflict-Born Child Receives First Vaccines

In Ethiopia, an estimated 3.9 million children have not received a single routine vaccine. These “zero-dose” children…

2 weeks ago