News

NAIBU WAZIRI WA AFYA DKT. MOLLEL AKABIDHI VYANDARUA KWA WANAWAKE SHINYANGA MJINI

Katika kuadhimisha siku ya Malaria Duniani, Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel ameungana na mwenyeji wake Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe Pascal Patrobas Katambi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini kugawa vyandarua kwa wanawake zaidi ya 400 pamoja na kufikia makundi mbalimbali ya wananchi katika jamii ndani ya Manispaa ya Shinyanga.

Dkt. Mollel ameipongeza Taasisi ya Doris Mollel kwa kushirikiana na Amref kuja na mkakati huo wa kuwafikia wananchi moja kwa moja na kuweza kutoa misaada mbalimbali inayogusa maisha ya Watanzania.

Naibu waziri wa afya dkt. Mollel akabithi vyandarua kwa wanawake Shinyanga mjini

Katika Warsha iliyohudhuriwa na wanawake zaidi ya 400, Dkt. Mollel amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imelenga kuboresha huduma za uzazi, mama na mtoto na kuhakikisha jamii inapata elimu ya kutosha na kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.

“Asante wakina mama mliokuja hapa kupata elimu ili mkatusaidie kuelimisha wengine na kupunguza vifo vya akina mama na watoto” amepongeza Dkt. Mollel

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Doris Mollel Bi. Doris Mollel amesema kuwa lengo la warsha hiyo ni kutoa elimu ya ugonjwa malaria na namna ya kujikinga pamoja na kuhamasisha wanawake kujitokeza kupata chanjo ya UVIKO-19 ili waweze kujikinga janga hili kubwa la korona, tunaliona linaisha ila bado ugonjwa upo.

“Zoezi limefanyika katika mikoa mitatu kwa kushirikiana na Amref kwa mikoa ya Simiyu, Kagera na Shinyanga na tunaishukuru Serikali kwa kutuwekea mazingira wezeshi sisi taasisi binafsi kuweza kufanya kazi na kutoa mchango wetu ndani ya jamii” amesema Doris Mollel.

Article first published on https://issamichuzi.blogspot.com/2022/04/naibu-waziri-wa-afya-dkt-mollel.html

Amref Health Africa

Amref Health Africa teams up with African communities to create lasting health change.

Recent Posts

Let’s recommit to strategies for a malaria-free, equitable world by 2030

Today provides an opportunity for the global community to reflect on the progress made in…

7 hours ago

How innovation and Collaboration will transform Turkana Children’s future

Kenya’s largest county by landmass sprawls across the north-western corner, enveloping nearly 77,000 square kilometres…

7 hours ago

Harvesting Hope: Transforming Health of Communities through Kitchen Gardening in South Suda

Step into the heart of South Sudan, where a powerful movement is taking root through…

3 days ago

Uzazi Salama Programme Launches in Kilifi County

The KES 225 Million investment aims to impact 500,000 lives by supporting reproductive, maternal, neonatal,…

6 days ago

African campaigner calls for targeted interventions to eliminate malaria

NAIROBI, April 25 (Xinhua) -- The goal of eliminating malaria in Africa by 2030 can…

6 days ago

Does Africa need a rethink on tackling violent extremism?

African leaders meeting at a security summit in Nigeria say the continent needs a new…

7 days ago