Coronavirus disease (COVID-19) News

Vijana Wahimizwa Wajitokeze Kwa Wingi Kupata Chanjo

NA LAWRENCE ONGARO

IDARA ya afya ya umma inalenga kuwapa chanjo vijana ambao kwa kawaida ndio wengi kwa idadi katika Kaunti ya Kiambu.

Mkurugenzi wa afya ya umma Bi Teresa Kariuki, alieleza kuwa hata ingawa wamepiga hatua kwa kuchanja wakazi wa Kiambu bado idadi kubwa ya vijana wanastahili kupata chanjo hiyo dhidi ya Covid-19.

Alisema kwa wakati huu wanalenga kufikia asilimia 40 ya vijana ambao wengi wao hawajapokea chanjo hiyo.

“Kwa muda mrefu kumekuwa na changamoto kwa vijana kujitolea wenyewe kwenda kuchanjwa hospitalini, na kwa hivyo tunatafuta njia mwafaka ya kuwafikia,” alifafanua mkurugenzi huyo.

Mkutano huo pia ulifadhiliwa na shirika la masuala ya afya la AMREF.

Aliyasema hayo mnamo Alhamisi eneo la Juja katika hafla iliyojumuisha washika dau wapatao 60 kutoka sekta mbalimbali.

Alieleza kuwa ilikuwa ni muhimu kufanya mkutano huo ili kuelewa changamoto zinazopatikana katika sekta hizo kuhusiana na maswala ya chanjo dhidi ya Covid-19.

Baadhi ya walioshiriki kwenye hafla hiyo walieleza dhana tofauti zinazosambazwa kwa wananchi kuwa inadhuru miili ya watu kwa njia moja ama nyingine.

Kulingana na takwimu ulitolewa na idara ya afya ya umma, katika kaunti ya Kiambu watu wapatao 1,124,753 milioni tayari wamepata chanjo ya Covid-19 ilipofika mwezi Disemba 2021.

Hata hivyo kufikia wakati huo pia watu wapatao 2,650 walikuwa wameambukizwa na homa ya Covid-19.

Hiyo ni kama asilimia 41.4 kwa wanaume na 58.7 kwa wanawake.

Kulingana na mkurugenzi huyo, wamezindua mbinu mpya watakayotumia ili kuwashawishi vijana waweze kupokea chanjo dhidi ya Covid-19.

Alisema watasajili vijana wenzao ili kuwarai kuchanjwa katika makanisa, na hata viwanjani wanakoshiriki michezo mbalimbali.

Alieleza pia watatumia mitandao, na burudani za muziki ili kuwaleta karibu vijana hao.

“Tumejaribu kwa muda mfupi na tumepata matokeo ya kuridhisha kwa kuwaleta karibu vijana hao,” alifafanua mkurugenzi huyo.

Katika hafla hiyo waandishi wa habari pia walihimizwa kuwa mstari wa mbele kuangazia yote yanayotendeka kuhusiana na janga la Covid-19 ili wananchi waelewe ukweli wa mambo.

“Tunaelewa vyema ya kwamba waandishi wa habari wana jukumu kubwa la kuangazia mengi kuhusu maswala ya covid-19 ili kila mwananchi aelewe umuhimu wa kuchanjwa,” alieleza mkurugenzi huyo.

Alisema hata ingawa kuenea kwa homa ya Covid-19 kunaendelea kupungua, lakini ni vyema watu kuendelea kuwa makini na kujichunga kwa kufuata maagizo yote ya idara husika za afya “ili tukabiliane nayo ipasavyo.”

Article first published on https://taifaleo.nation.co.ke/covid-19-vijana-wahimizwa-wajitokeze-kwa-wingi-kupata-chanjo/

Amref Health Africa

Amref Health Africa teams up with African communities to create lasting health change.

Recent Posts

Let’s recommit to strategies for a malaria-free, equitable world by 2030

Today provides an opportunity for the global community to reflect on the progress made in…

3 days ago

How innovation and Collaboration will transform Turkana Children’s future

Kenya’s largest county by landmass sprawls across the north-western corner, enveloping nearly 77,000 square kilometres…

3 days ago

Harvesting Hope: Transforming Health of Communities through Kitchen Gardening in South Suda

Step into the heart of South Sudan, where a powerful movement is taking root through…

6 days ago

Uzazi Salama Programme Launches in Kilifi County

The KES 225 Million investment aims to impact 500,000 lives by supporting reproductive, maternal, neonatal,…

1 week ago

African campaigner calls for targeted interventions to eliminate malaria

NAIROBI, April 25 (Xinhua) -- The goal of eliminating malaria in Africa by 2030 can…

1 week ago

Does Africa need a rethink on tackling violent extremism?

African leaders meeting at a security summit in Nigeria say the continent needs a new…

1 week ago